DEAR GRANDPA*******
Ni safari ya maisha chini ya mbingu, udai kuzaliwa majaliwa, kuishi bahati kutunikiwa kifikia hitimisho uwa sio kikomo cha kusafiria nyota yako mbali ni pumziko kuanza maisha mapya ya ufunuo.
chini ya mbingu na ardhi yapo mengi Ila mbinguni upo uzima wa milele, mtu si kitu Ila ubinadamu ndo utu utazamwa vitendo sio maneno tu....... twajua kupenda Ila mola akipenda zaidi hatuna budi Ila kulieshimu angano panapobidi, upo wakati wa kila tukio. kupanda na kuvuna ,kutawanya kukusanya, yote yameandikwa na kalamu ya wino usofutika. kama kiumbe utahisi vipi ukiachwa na aliyekupa uhai na moyo kuishi? uwa ni wakati mgumu ni kama kukosa kipande cha nafsi ........uhuru wa nafsi ujanzwa na upendo ulojawa na hekima********
*Ni wiki tatu zimepita toka nipokee simu yako, kunipa agano lako la mwisho baada kulihabiri jahazi la maisha miaka mingi. sikutarajia muda ulikuwa ushawadia kuliengesha dau la maisha ukingoni ,ni bahari ya maisha na sote tuwasafiri...... dunia mapito! udai waraka nusu ya kuonana,***** dhaabu maarifa zipo Ila midomo inenayo maarifa johari isopatikana...... umekuwa nguzo maishani mwangu kwa mema malezi na mafunzo sitokusahau umelala usingizi usonjua wakati wa kuamka..... kimwili hatupo nawe Ila akili nafsi na moyoni upo. naaminia ipo siku tutajapatana ya chini ya mbingu tutakumbushana
funzo kuu kwa mjukuu ulonipa kutii agano la mwenyezi mungu......... masomo mengi ya maisha ulinifundisha, nayaifadhi akilini mwangu.....' kama nyota ya alfajiri kiumbe nahitaji kung'aa...... kama uzima wa milele uwe wangu ufunuo .........kama enzi za nitume niadhimishe langu agano .......mbele ya kiti cha enzi nivishwe langu taji..... dua njema nakusalia mola akuweke pema peponi kwa hekima Penye njia bila udhia ipo njia...... yalipo malengo na mwelekeo kufikia
hekima yako imeniingia moyoni......... maarifa yakanipendeza nafsi..... busara itanilinda ufahamu utaniifadhi..... nashukuru mungu umekuwa mwalimu wangu wa mawaidha miahani mwangu pengo uloliwacha moyoni mwangu hakuna wa kuliziba*********on 20th my grandpa died after i travelled back R.I.P....DAVID M.MUTHUKUI... what you have just read is my letter to him ************my grandpa meant love to me ******i seen no other lover in life
Site Options
1 Comment
Add CommentCliff Lyon wrote:
My thoughts are with you and for grandpa. :)